International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi, May 02 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 May 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi, May 02 2026

Dirisha la usajili linaendelea kupamba moto huku vilabu vikubwa vikianza kupanga mustakabali wa vikosi vyao kuanzia kushusha nyota wapya na kuwekeza kwa vipaji chipukizi. Leo Jumamosi, Mei 2, 2026, tetesi zimejaa mipango ya muda mrefu, ushindani mkali, na majina makubwaΒ 


Barcelona wamvizia Joao Pedro

Barcelona wameanza kumfuatilia Joao Pedro (24) wa Chelsea kama mbadala wa muda mrefu wa Robert Lewandowski (37).

Nyota huyo amewekwa juu ya orodha ya washambuliaji wanaoweza kuziba pengo hilo.
Chanzo: Marca


Aston Villa wafuatilia kijana wa PSG

Aston Villa wanamfuatilia mshambuliaji chipukizi Ibrahim Mbaye (18) wa Paris Saint-Germain.

Hii inaonyesha mwelekeo wa Villa kuwekeza zaidi kwa vijana.
Chanzo: Daily Mail


Barcelona wamuweka Romero kama mbadala

Barcelona wanaweza kumgeukia Cristian Romero (Tottenham Hotspur) iwapo watashindwa kumsajili Alessandro Bastoni wa Inter Milan.
Chanzo: AS


Aston Villa wamuuza Tommi O'Reilly

Aston Villa wako tayari kumuuza Tommi O'Reilly (22), ambaye yuko kwa mkopo Crewe Alexandra.

Vilabu vinavyomtaka:

  • Oxford United
  • Portsmouth
  • Huddersfield Town

Chanzo: Daily Mail


Coventry na Leeds wamuwania Lois Openda

Coventry City watapambana na Leeds United kumsajili Lois Openda (26).

Kwa sasa anacheza kwa mkopo Juventus kutoka RB Leipzig.
Chanzo: Sport Witness


Bayern Munich wamvizia Anthony Gordon

Wawakilishi wa Anthony Gordon (25) wa Newcastle United wamekuwa kwenye mazungumzo na Bayern Munich kwa miezi kadhaa.

Kocha Vincent Kompany ameridhia uwezekano huo.
Chanzo: Florian Plettenberg


Hayden Hackney aingia kwenye rada ya Brighton

Hayden Hackney (23) wa Middlesbrough anawindwa na:

  • Brighton & Hove Albion
  • Nottingham Forest

Chanzo: Football Insider


Vita ya kumsajili Bailey Rice

Bailey Rice (19) wa Rangers anawindwa na:

  • Nottingham Forest
  • Aston Villa
  • Crystal Palace

Chanzo: Teamtalk


Aston Villa wamkaribia James Trafford

Aston Villa wanatarajiwa kuongeza juhudi za kumsajili James Trafford (23) wa Manchester City kama mbadala wa Emiliano Martinez.
Chanzo: Football Insider


Hansi Flick kuongeza mkataba Barcelona

Kocha wa Barcelona, Hansi Flick (61), anatarajiwa kuongeza mkataba wa miaka miwili.
Chanzo: Mundo Deportivo

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’