Makocha Simba, Yanga wafunguka maandalizi ya Kariakoo Derby

Joel JJ By Joel JJ • 2nd May 2026


Makocha Simba, Yanga wafunguka maandalizi ya Kariakoo Derby

Msisimko wa dabi ya Kariakoo unazidi kupamba moto kuelekea pambano kali kati ya Simba SC na Yanga litakalopigwa Jumapili May 03 katika uwanja wa Isamuhyo.

Makocha wa timu zote mbili leo wakifunguka kuhusu maandalizi ya timu zao kuelekea mchezo huo mkubwa wa Ligi Kuu ya NBC.


Gonçalves: Tuko tayari kwa mpango tofauti

Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Gonçalves, amesema maandalizi ya kikosi chake yanaendelea vizuri na wamebakiza hatua za mwisho kabla ya mchezo wa Jumapili.

Ameeleza kuwa timu imepata siku tatu za maandalizi maalum na sasa wanakamilisha mikakati ya mwisho kuelekea pambano hilo muhimu.

“Tumekuwa na siku tatu za maandalizi kuelekea mchezo wa Jumapili. Huu ni mchezo wa ligi hivyo tumejiandaa na mpango tofauti,” alisema Gonçalves.

“Leo tutakuwa na maandalizi ya mwisho ya kimkakati. Tunasikitika hatukupata matokeo mazuri kwenye mchezo uliopita lakini naamini tuko katika njia sahihi.”

Kocha huyo ameongeza kuwa wanatarajia mchezo mgumu lakini wenye matokeo chanya kwa upande wao, huku akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kuisapoti timu.

“Tuna matumaini makubwa ya kufanya vizuri kesho. Mashabiki wetu waje kwa wingi kutuunga mkono. Hii ni nafasi muhimu kuongeza pengo la pointi.”

Gonçalves pia alizungumzia mchezo uliopita, akisema licha ya kutopata ushindi, aliridhishwa na kiwango cha wachezaji wake. Hata hivyo, alionesha kusikitishwa na kukosekana kwa kiungo Mudathir Yahya kutokana na adhabu ya kufungiwa, akilinganisha na hali ya mchezaji wa Simba aliyeonekana kutoadhibiwa kabla ya mchezo uliozikutanisha timu hizo March 1.

Hata hivyo, ameweka wazi kuwa Yanga haitategemea mchezaji mmoja na tayari kuna mbadala wa nafasi hiyo.


Barker: Tunahitaji ushindi ili kubaki kwenye mbio za ubingwa

Kwa upande wa Simba, kocha Steve Barker amesema mchezo wa kesho ni muhimu sana kwa mustakabali wa ubingwa wa msimu huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Barker alisisitiza kuwa kushinda Yanga ni lazima ikiwa Simba wanataka kuendelea kubaki kwenye mbio za taji.

“Kama tukipoteza mchezo dhidi ya Yanga, nafikiri matarajio ya ubingwa yatakuwa magumu zaidi,” alisema.

“Tunahitaji kushinda, hasa tukiwa uwanja wa nyumbani. Matokeo hayo yatatuweka katika nafasi nzuri.”

Ameongeza kuwa anatarajia mchezo mgumu lakini anaamini kikosi chake kiko tayari kupambana kwa nguvu zote, huku akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kuisapoti timu.

“Sisi ni Simba na tuko tayari kupambania kila alama,” alisisitiza Barker.


Simba na Yanga zinakutana katika mchezo huo muhimu wa ligi zikiwa zimepita takribani siku tano tangu timu hizo zilipokutana kwenye mchezo wa fainali kombe la Muungano Simba ikiibuka na ushindi katika mchezo huo uliopigwa kwa dakika 120.

Wakati huu timu hizo zinakutana huku kila moja ikihitaji alama tatu, Yanga wanaweza kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa kama watashinda mchezo huo wakati Simba ushindi utaweka matumaini hai kwenye mbio za ubingwa kwani watapunguza gap la pointi kutoka tano hadi mbili lakini wakifungwa zitakuwa nane.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →