Local,Normal News,Kenya, Uganda, Tanzania, Pamoja

Droo ya kufuzu Afcon 2027 yapangwa May 19

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 May 2026
Droo ya kufuzu Afcon 2027 yapangwa May 19

Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) limethibitisha rasmi kuwa droo ya michuano ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 itafanyika tarehe 19 Mei 2026, hatua itakayoweka ramani ya safari ya mataifa 48 yanayowania nafasi ya kushiriki fainali za AFCON PAMOJA 2027.

Kwa mujibu wa CAF, droo hiyo itahusisha jumla ya timu 48, ikiwa ni pamoja na wenyeji wenza wa mashindano hayo, Kenyha, Tanzania na Uganda ambao tayari wamefuzu moja kwa moja kama wenyeji wa fainali hizo zitakazofanyika kwa pamoja katika nchi hizo tatu za Afrika Mashariki.

Mfumo wa makundi

Katika droo hiyo, timu 48 zitapangwa kwenye makundi 12, kila kundi likiwa na timu nne. Kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa, timu mbili za juu katika kila kundi zitafuzu moja kwa moja kwenda fainali za AFCON 2027.

Mfumo huo unatarajiwa kuongeza ushindani mkubwa, ambapo kila mchezo wa kufuzu utakuwa na umuhimu wa moja kwa moja katika kuhakikisha timu inasonga mbele au kuondolewa katika mbio za kufuzu.

Ratiba ya mechi za kufuzu

CAF pia imetangaza vipindi vitakavyotumika kwa mechi za hatua ya makundi kama ifuatavyo:

  • Septemba hadi Oktoba 2026
  • Novemba 2026
  • Machi 2027

Vipindi hivyo vitatumika kukamilisha ratiba ya timu zitakazofuzu na kujiunga na mataifa wenyeji katika fainali za 2027.

AFCON PAMOJA 2027

Michuano ya AFCON 2027, maarufu kama AFCON PAMOJA 2027, itakuwa ya kihistoria kwa kuwa itafanyika kwa mara ya kwanza katika mataifa matatu kwa pamoja ya Afrika Mashariki. Mashindano hayo yanatarajiwa kuongeza hadhi ya soka katika ukanda huo na kuvutia mashabiki kutoka pembe zote za dunia.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
7h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
16h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’