Local,Normal News,Azam, Mtibwa, Coastal, Singida

Fei Toto hakamatiki, afunga mawili Azam Fc ikiichapa Mtibwa Sugar 3-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 May 2026
Fei Toto hakamatiki, afunga mawili Azam Fc ikiichapa Mtibwa Sugar 3-0

Leo Jumamosi, Mei 02, 2026, mashabiki wa soka nchini walishuhudia michezo miwili ya ligi kuu ya NBC, yenye ushindani mkali huku timu zikionyesha dhamira ya kusaka alama muhimu.

Katika dimba la KMC Complex, mapema Mtibwa Sugar walikaribisha Azam FC katika mchezo uliotawaliwa na wageni. Azam FC waliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0, wakionyesha ubora mkubwa kuanzia dakika za mwanzo hadi mwisho wa mchezo.

Nyota wa mchezo huo alikuwa Feisal Salum maarufu kama Fei Toto, aliyefunga mabao mawili na pia kutoa pasi ya bao kwa Japhet Kitambala.

Kwa mafanikio hayo, Feisal sasa anaongoza orodha ya wafungaji bora akifikisha mabao 9, huku pia akiwa ametoa pasi 8 za mabao, takwimu zinazoonyesha mchango wake mkubwa ndani ya kikosi cha Azam FC kwa msimu wa tatu mfululizo.

Wakati huo huo, katika mchezo mwingine uliokuwa na ushindani mkubwa, Coastal Union waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars. Licha ya kucheza pungufu baada ya kupata kadi nyekundu kwa mlinda lango, Coastal Union waliweza kuhimili presha na kuhakikisha wanabeba alama zote tatu.

Mabao ya Coastal Union yalifungwa na Bakari Msimu pamoja na Mabad Maulid aliyefunga kwa njia ya penati. Kwa upande wa Singida BS, bao lao pekee lilifungwa na Emmanuel Keyekeh kupitia mkwaju wa penati.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’