Real Madrid waichelewesha Barcelona kutangaza ubingwa La Liga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th May 2026


Real Madrid waichelewesha Barcelona kutangaza ubingwa La Liga

Real Madrid wamefanikisha kazi yao ya kuchelewesha sherehe za ubingwa kwa wapinzani wao wakubwa Barcelona baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Espanyol Jumapili, Mei 3, 2026.

Katika mechi hiyo ya La Liga iliyochezwa kwa ushindani mkali, Real Madrid walionyesha uimara wao na kutumia nafasi walizopata, Vinicios Junior akifunga mabao yote na kuhakikisha wanachukua pointi zote tatu muhimu ugenini.

Ushindi huo unamaanisha kuwa Barcelona bado hawajaweza kutangazwa mabingwa rasmi wa ligi hiyo, licha ya kuwa karibu na taji hilo msimu huu.

Madrid walionekana kuingia uwanjani wakiwa na dhamira moja kuu kutokubali kupoteza au kutoa nafasi yoyote ambayo ingewasaidia Barcelona kutwaa ubingwa mapema.

Mashabiki na wachambuzi wa soka nchini Hispania wanasema matokeo hayo yanaongeza ladha ya ushindani kuelekea mchezo unaosubiriwa kwa hamu wa El Clásico, ambao sasa unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuamua hatima ya ubingwa wa ligi msimu huu.

Kama Real Madrid watakosa ushindi kwenye El Classico basi Barcelona watatawazwa kuwa mabingwa wa La Liga kwa msimu wa pili mfululizo


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’