International,Real Madrid, Barcelona, Espanyol, Local

Real Madrid waichelewesha Barcelona kutangaza ubingwa La Liga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 May 2026
Real Madrid waichelewesha Barcelona kutangaza ubingwa La Liga

Real Madrid wamefanikisha kazi yao ya kuchelewesha sherehe za ubingwa kwa wapinzani wao wakubwa Barcelona baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Espanyol Jumapili, Mei 3, 2026.

Katika mechi hiyo ya La Liga iliyochezwa kwa ushindani mkali, Real Madrid walionyesha uimara wao na kutumia nafasi walizopata, Vinicios Junior akifunga mabao yote na kuhakikisha wanachukua pointi zote tatu muhimu ugenini.

Ushindi huo unamaanisha kuwa Barcelona bado hawajaweza kutangazwa mabingwa rasmi wa ligi hiyo, licha ya kuwa karibu na taji hilo msimu huu.

Madrid walionekana kuingia uwanjani wakiwa na dhamira moja kuu kutokubali kupoteza au kutoa nafasi yoyote ambayo ingewasaidia Barcelona kutwaa ubingwa mapema.

Mashabiki na wachambuzi wa soka nchini Hispania wanasema matokeo hayo yanaongeza ladha ya ushindani kuelekea mchezo unaosubiriwa kwa hamu wa El Clásico, ambao sasa unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuamua hatima ya ubingwa wa ligi msimu huu.

Kama Real Madrid watakosa ushindi kwenye El Classico basi Barcelona watatawazwa kuwa mabingwa wa La Liga kwa msimu wa pili mfululizo

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
14m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’