Mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England zimechukua sura mpya baada ya Manchester City kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Everton katika mchezo uliopigwa Jumatatu usiku dimba la Goodson Park.
Matokeo hayo yameipa Arsenal faida kubwa kileleni mwa msimamo wa Premier League, huku sasa wakihitaji kushinda mechi zao zilizobaki ili kujihakikishia ubingwa bila kutegemea timu nyingine.



