Local,Normal News,Yanga, KMC

Goncalves apania alama tatu dhidi ya KMC

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 May 2026
Goncalves apania alama tatu dhidi ya KMC

Kocha Mkuu wa Yanga Pedro Goncalves amesema kikosi chake leo kinarejea mazoezini kukamilisha maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC utakaopigwa kesho Jumatano katika uwanja wa KMC Complex.

Akizungumza katika mkutano na wanahabari mapema leo, Goncalves amesema alitoa mapumziko ya siku moja kwa wachezaji wake baada ya wiki mbili za mfululizo wa mechi.

Kocha huyo raia wa Ureno amesema wanakwenda kuikabili KMC kwa umakini mkubwa lengo lao likiwa kuibuka na ushindi.

"Leo tunarudi kambini kufanya maandalizi ya Mchezo wetu wa kesho dhidi ya KMC, Jana tuliwapa wachezaji Mapumziko baada ya kuwa na wiki mbili kambini ili kujiweka sawa, Tunaamini maandalizi yetu ya leo yatatupa kitu kizuri ili kuhakikisha tunakusanya alama tatu hapo kesho"

Haijalishi tunacheza na nani, lengo letu ni kukusanya alama tatu kwenye kila mchezo, hivyo tutakuwa makini na tutawaheshimu KMC huku tukiingia na malengo yetu ya kushinda mchezo

"Nafahamu kuwa KMC watakuja na Morali kubwa kwasababu wanataka kukusanya alama ili kujiweka sehemu nzuri, watakuja kwa kutuheshimu kwasababu wanacheza na timu inayoongoza ligi, lakini Sisi tutajitoa kwa asilimia mia moja ili kushinda mechi hii," alisema Goncalves.

Yanga ndio vinara wa ligi wakiwa na alama 48 baada ya mechi 20, kimahesabu wanahitaji kushinda angalau mechi 9 kati ya 10 zilizobaki ili kutetea ubingwa kwa msimu wa tano mfululizo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’