International,Normal News,Zamalek, Pyramids, Al Ahly, Local

Mechi ya mwisho kuamua Bingwa Misri: Zamalek, Pyramids na Al Ahly

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2026
Mechi ya mwisho kuamua Bingwa Misri: Zamalek, Pyramids na Al Ahly

Mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Misri zimefikia hatua ya mwisho ya kusisimua zaidi, ambapo mshindi wa msimu wa 2025/2026 ataamuliwa katika siku ya mwisho ya ligi, Mei 20, katika ushindani mkali kati ya Zamalek SC, Pyramids FC na Al Ahly SC.

Huu ni msimu wa kipekee katika historia ya ligi hiyo, ambapo timu tatu zinaingia katika mechi za mwisho zikiwa bado na nafasi ya kutwaa ubingwa, huku mechi zote muhimu zikitarajiwa kuchezwa kwa wakati mmoja.

Zamalek SC wako katika nafasi nzuri zaidi ya kutwaa taji hilo, wana alama 53 wakihitaji pointi moja tu katika mchezo wao dhidi ya Ceramica Cleopatra ili kutangazwa mabingwa wa ligi. Matokeo ya ushindi au sare yatawatosha kumaliza msimu kileleni.

Kwa upande wa Pyramids FC, wao wana alama 51, wanahitaji kushinda dhidi ya Smouha, huku wakisubiri Zamalek wapoteze mchezo wao ili waweze kutwaa ubingwa.

Al Ahly SC, mabingwa wa kihistoria wa soka la Misri, wana alama 50, bado wana nafasi ya kutetea taji hilo, lakini wanahitaji mchanganyiko mgumu zaidi wa matokeo. Wanatakiwa kushinda dhidi ya Al Masry, Zamalek wapoteze, na Pyramids wapate sare ili wao waibuke mabingwa.

Kinachofanya msisimko huo kuwa mkubwa zaidi ni ukweli kwamba mechi zote tatu zitapigwa kwa wakati mmoja, hali itakayowafanya mashabiki kufuatilia matokeo kutoka viwanja tofauti kwa wakati mmoja, huku kila bao likiwa na athari ya moja kwa moja kwenye mbio za ubingwa.

Kuna uwezekano mkubwa Al Ahly msimu huu wakamaliza katika nafasi ya tatu kama timu zote zitashinda mechi zao za mwisho. Ikiwa hivyo Al Ahly watacheza michuano ya kombe la Shirikisho (CAFCC) baada ya misimu mingi ya kutawala ligi ya mabingwa (CAFCL).

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’