Local,Normal News,Yanga

Goncalves afutwa kazi Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2026
Goncalves afutwa kazi Yanga

Uongozi wa Klabu ya Yanga umetangaza rasmi kumfuta kazi aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Pedro Goncalves, raia wa Ureno.

Taarifa hiyo imetolewa muda mfupi baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya KMC uliochezwa katika dimba la KMC Complex, ambapo Yanga iliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0.

Licha ya kupata alama tatu muhimu, inaelezwa kuwa uongozi wa klabu haukuridhishwa na mwenendo wa timu kwa ujumla.

Katika mabadiliko hayo ya benchi la ufundi, Kocha Msaidizi Abdulhamid Moarin amepewa jukumu la kuiongoza timu akisaidiana na Patrick Mabedi hadi mwishoni mwa msimu.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha timu inaendelea kuwa katika ushindani huku klabu ikitafakari mustakabali wa benchi la ufundi.

Goncalves alijiunga na Yanga kwa matarajio makubwa, lakini matokeo na kiwango cha timu katika baadhi ya michezo yameonekana kuwa chini ya matarajio ya mashabiki na uongozi.

More Stories

Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
9m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
40m ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
1h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
8h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
13h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
13h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
15h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
15h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
19h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
21h ago
READ MORE β†’