Local,Normal News,Simba, JKT

Simba yarudi nafasi ya pili, yaichapa JKT Tanzania 1-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2026
Simba yarudi nafasi ya pili, yaichapa JKT Tanzania 1-0

Simba SC imefanikiwa kurejea katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kuichapa JKT Tanzania bao 1-0 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili, ambapo Simba walionekana kutawala mchezo kwa muda mwingi huku JKT Tanzania wakicheza kwa nidhamu ya hali ya juu ya kujilinda na kutegemea mashambulizi ya kushitukiza.

Licha ya kutengeneza nafasi kadhaa muhimu katika kipindi cha kwanza, Simba walishindwa kuzitumia ipasavyo na iliwabidi kusubiri hadi kipindi cha pili kupata bao la ushindi kupitia kwa Clatous Chama, ambaye aliendelea kuonyesha mchango wake muhimu katika kikosi hicho.

Kiungo mshambuliaji Elie Mpanzu aliendeleza makali yake baada kuandikisha asisti nyingine muhimu, akimtengenezea Chama bao hilo ikiwa ni muendelezo wa ushirikiano wao mzuri kama ilivyoshuhudiwa katika mchezo uliopita dhidi ya Yanga.

Kipindi cha pili JKT Tanzania walionekana kuongeza kasi na kujaribu kurejea mchezoni, lakini Simba waliimarisha safu yao ya ulinzi na kudhibiti mashambulizi hayo hadi mwisho wa mchezo.

Kwa ushindi huo, Simba imefikisha alama 46 na kurejea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi, ikiiangusha Azam FC ambayo sasa imeshuka hadi nafasi ya tatu.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
6h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’