Enrique akiri haikuwa rahisi kuitoa Bayern Munich

Joel JJ By Joel JJ โ€ข 7th May 2026


Enrique akiri haikuwa rahisi kuitoa Bayern Munich

Kocha mkuu wa Paris Saint-Germain (PSG), Luis Enrique, amesema Bayern Munich ndiyo timu iliyompa wakati mgumu zaidi katika safari yao ya kuelekea fainali ya UEFA Champions League msimu huu.

Enrique ametoa kauli hiyo baada ya PSG kufuzu kucheza fainali kwa kuiondoa Bayern Munich kwa jumla ya mabao 6-5 kufuatia sare ya 1-1 kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa Allianz Arena nchini Ujerumani.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Luis Enrique alikiri kuwa Bayern ilikuwa moja ya timu hatari zaidi walizokutana nazo kutokana na ubora wao wa kushambulia na presha kubwa waliyoitoa katika michezo yote miwili ya nusu fainali.

Enrique ameweka wazi kuwa alikuwa akihofia uwezo wa Bayern hasa kutokana na kasi yao ya kushambulia na uzoefu mkubwa waliokuwa nao katika michuano hiyo.

Hata hivyo, kocha huyo amesema hana hofu yoyote kuelekea mchezo wa fainali dhidi ya Arsenal utakaopigwa Budapest mwishoni mwa mwezi huu.

Luis Enrique amesema PSG imeonyesha uwezo mkubwa wa kucheza dhidi ya timu bora Ulaya na ana imani kikosi chake kiko tayari kutetea ubingwa wao wa Ulaya dhidi ya Arsenal.

PSG imefika fainali ya pili mfululizo ya UEFA Champions League baada ya kutwaa taji hilo mwaka 2025 kwa kuichapa Inter Milan mabao 5-0 katika fainali ya kihistoria.

Kwa upande wa Arsenal, timu hiyo imefanikiwa kutinga fainali baada ya kuitoa Atletico Madrid na sasa itakuwa ikisaka taji lake la kwanza kabisa la UEFA Champions League katika historia ya klabu hiyo.

Fainali ya UEFA Champions League 2026 inatarajiwa kupigwa Mei 30 katika dimba la Puskรกs Arรฉna mjini Budapest, Hungary, huku PSG ikisaka kuwa timu ya kwanza kutetea taji hilo tangu Real Madrid walivyofanya mwaka 2018.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE โ†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE โ†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE โ†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE โ†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE โ†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE โ†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE โ†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE โ†’