Moalin apania ushindi wa kwanza dhidi ya Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ โ€ข 8th May 2026


Moalin apania ushindi wa kwanza dhidi ya Coastal Union

Kocha Mkuu mpya wa Yanga, Abdilhamid Moalin, amesema yupo tayari kuanza kazi rasmi kwa ushindi pale timu yake itakaposhuka dimbani kesho kuivaa Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kwenye KMC Complex.

Moalin ambaye amekabidhiwa mikoba iliyoachwa na Pedro Goncalves, amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika kwa kiwango kizuri huku akionesha kujiamini kuwa kikosi chake kitaonyesha kiwango bora mbele ya mashabiki wa Yanga.

Kocha huyo wa zamani wa Azam FC na KMC FC amesema wachezaji wote wako tayari kwa pambano hilo muhimu na wanaelewa matarajio makubwa ya mashabiki wa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu.

โ€œMaandalizi ya mchezo wa Coastal Union yamefanyika salama. Kila mchezaji yupo imara kukabiliana na mchezo huo. Nina matumaini na vijana wetu kuwa watatupatia kila kilicho bora. Ukweli ni kwamba vijana wanajua mashabiki wanataka nini. Kila mchezaji anapaswa kuweka akili yake kwenye mchezo wa kesho,โ€ alisema Moalin.

Mbali na kuahidi ushindi, Moalin amesema mashabiki wa Yanga wanapaswa kutarajia kuona timu yao ikicheza soka la kushambulia na kumiliki mchezo kwa dakika zote 90.

โ€œKitu ninachoweza kuwaahidi mashabiki wa Yanga ni mchezo mzuri. Sisi kama Yanga tuna namna yetu ya mchezo. Msingi wa Yanga ni kumiliki mchezo. Tunawaheshimu Coastal Union lakini hatuwezi kuacha utamaduni wetu. Tunataka kumiliki dimba, sio kwa dakika chache bali kwa dakika zote 90,โ€ aliongeza.

Aidha, kocha huyo amesisitiza kuwa licha ya kujiamini, hawaichukulii poa Coastal Union kutokana na ubora wa kikosi hicho, huku akieleza kuwa bado ana muda mchache wa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya timu tangu achukue majukumu hayo mapya.

โ€œNiwe mkweli, Coastal Union ni timu nzuri. Tunawaheshimu sana kama ambavyo tunaheshimu wapinzani wengine. Vijana wetu wanaelewa kabisa kuwa huu sio mchezo rahisi. Tuna muda mchache sana wa kubadilisha vitu kwenye timu yetu. Tutatumia muda mchache uliopo kurekebisha machache yanayorekebishika,โ€ alisema.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE โ†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE โ†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE โ†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE โ†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE โ†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE โ†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE โ†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE โ†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE โ†’