Local,Normal News,Yanga, Coastal

Moalin apania ushindi wa kwanza dhidi ya Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ
8 May 2026
Moalin apania ushindi wa kwanza dhidi ya Coastal Union

Kocha Mkuu mpya wa Yanga, Abdilhamid Moalin, amesema yupo tayari kuanza kazi rasmi kwa ushindi pale timu yake itakaposhuka dimbani kesho kuivaa Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kwenye KMC Complex.

Moalin ambaye amekabidhiwa mikoba iliyoachwa na Pedro Goncalves, amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika kwa kiwango kizuri huku akionesha kujiamini kuwa kikosi chake kitaonyesha kiwango bora mbele ya mashabiki wa Yanga.

Kocha huyo wa zamani wa Azam FC na KMC FC amesema wachezaji wote wako tayari kwa pambano hilo muhimu na wanaelewa matarajio makubwa ya mashabiki wa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu.

“Maandalizi ya mchezo wa Coastal Union yamefanyika salama. Kila mchezaji yupo imara kukabiliana na mchezo huo. Nina matumaini na vijana wetu kuwa watatupatia kila kilicho bora. Ukweli ni kwamba vijana wanajua mashabiki wanataka nini. Kila mchezaji anapaswa kuweka akili yake kwenye mchezo wa kesho,” alisema Moalin.

Mbali na kuahidi ushindi, Moalin amesema mashabiki wa Yanga wanapaswa kutarajia kuona timu yao ikicheza soka la kushambulia na kumiliki mchezo kwa dakika zote 90.

“Kitu ninachoweza kuwaahidi mashabiki wa Yanga ni mchezo mzuri. Sisi kama Yanga tuna namna yetu ya mchezo. Msingi wa Yanga ni kumiliki mchezo. Tunawaheshimu Coastal Union lakini hatuwezi kuacha utamaduni wetu. Tunataka kumiliki dimba, sio kwa dakika chache bali kwa dakika zote 90,” aliongeza.

Aidha, kocha huyo amesisitiza kuwa licha ya kujiamini, hawaichukulii poa Coastal Union kutokana na ubora wa kikosi hicho, huku akieleza kuwa bado ana muda mchache wa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya timu tangu achukue majukumu hayo mapya.

“Niwe mkweli, Coastal Union ni timu nzuri. Tunawaheshimu sana kama ambavyo tunaheshimu wapinzani wengine. Vijana wetu wanaelewa kabisa kuwa huu sio mchezo rahisi. Tuna muda mchache sana wa kubadilisha vitu kwenye timu yetu. Tutatumia muda mchache uliopo kurekebisha machache yanayorekebishika,” alisema.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →