International,Normal News,World Cup, Local

Tramp akosoa bei ya tiketi kombe la Dunia

Joel JJ By Joel JJ
8 May 2026
Tramp akosoa bei ya tiketi kombe la Dunia

Rais wa Marekani, Donald Trump, ameibua mjadala mpya kuhusu bei za tiketi za michuano ya Kombe la Dunia 2026, akizielezea kuwa ni kubwa kupita kiasi na zisizowiana na uwezo wa mashabiki wa kawaida.

Akizungumza katika mahojiano na vyombo vya habari, Trump amesema haelewi sababu ya tiketi hizo kuuzwa kwa bei za juu kiasi hicho, akisisitiza kuwa hata yeye binafsi asingekuwa tayari kulipa gharama hizo ili kushuhudia mechi.

“Singeweza kulipa hizo bei, kusema kweli,” alinukuliwa Trump akisema, kauli iliyozua mjadala mpana kuhusu uhalisia wa gharama za mashindano hayo.

Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika kwa pamoja nchini Marekani, Canada na Mexico, limekuwa likikabiliwa na malalamiko kutoka kwa mashabiki na wadau wa soka kuhusu mfumo wa bei unaotumika, unaojulikana kama dynamic pricing, ambapo tiketi hupanda bei kulingana na mahitaji.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, baadhi ya tiketi za mechi za awali zimeuzwa kwa zaidi ya dola 1,000, huku mechi kubwa zikienda hadi maelfu ya dola, hali inayoibua hofu kuwa mashabiki wa kawaida wanaweza kushindwa kumudu kuhudhuria.

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeendelea kutetea mfumo huo, likisema bei zinaendana na thamani ya tukio na mahitaji makubwa ya kimataifa ya mashindano hayo, ambayo yanatarajiwa kuvunja rekodi ya mahudhurio.

Wakati mjadala huo ukiendelea, wadau mbalimbali wa soka wameitaka FIFA kufanya tathmini ya bei hizo ili kuhakikisha mashabiki wengi zaidi wanapata nafasi ya kushuhudia moja ya michuano mikubwa zaidi duniani.

Kombe la Dunia 2026 linatarajiwa kuanza Juni 2026, likiwa na mvuto mkubwa kimataifa lakini pia likigubikwa na mjadala mkali kuhusu gharama za tiketi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →