Local,Normal News,Simba, Prisons

Simba yaipigia hesabu kali Tanzania Prisons

Joel JJ By Joel JJ
9 May 2026
Simba yaipigia hesabu kali Tanzania Prisons

Kikosi cha Simba SC kinaendelea na maandalizi makali kuelekea mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Tanzania Prisons utakaopigwa Jumapili, May 10 katika dimba la KMC Complex jijini Dar es Salaam.

Wekundu wa Msimbazi wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na lengo moja tu la kuhakikisha wanapata alama tatu muhimu katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu msimu huu.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Simba, Suleiman Matola, amesema maandalizi ya timu yanaendelea vizuri huku wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri kuelekea pambano hilo.

“Maandalizi ya mchezo yamekamilika kwa kiasi kikubwa, wachezaji wote wako kwenye hali nzuri kuelekea mchezo huu. Tunajua hautakuwa mchezo mwepesi lakini tumejiandaa kupambana ili kupata alama tatu,” alisema Matola.

Matola ameweka wazi kuwa benchi la ufundi linautambua ubora wa Tanzania Prisons, lakini Simba imejipanga kuhakikisha haitoi nafasi ya kupoteza pointi katika kipindi hiki muhimu cha msimu.

Mchezo huo pia utakuwa wa kwanza kwa Simba kucheza katika uwanja wa KMC Complex kama uwanja wao wa nyumbani msimu huu baada ya kuhamia rasmi kutoka uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni.

Uamuzi wa kurejea KMC Complex umetokana na changamoto za hali ya hewa pamoja na matumizi makubwa ya uwanja wa Isamuhyo katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea jijini Dar es Salaam.

Kwa sasa Simba wanaonekana kuingia kwenye hatua muhimu ya mwisho ya msimu huku kila mchezo ukiwa na uzito mkubwa katika mbio za ubingwa. Mashabiki wa klabu hiyo wanatarajia kuona timu yao ikiendeleza kiwango kizuri na kuendelea kuweka presha kwa wapinzani wao kwenye msimamo wa ligi.

Simba pia wanatarajiwa kucheza mechi zao zote zilizosalia msimu huu katika dimba la KMC Complex huku matumaini yakiwa makubwa ya kumaliza msimu kwa nguvu.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →