Local,Normal News,Simba, Prisons, KMC, Fountan, Pamba, Dodoma

Simba yaifumua Prisons 4-0, KMC mambo magumu

Joel JJ By Joel JJ
10 May 2026
Simba yaifumua Prisons 4-0, KMC mambo magumu

Mikiki mikiki ya Ligi Kuu NBC imeendelea leo kwa michezo mitatu kupigwa katika viwanja tofauti huku vigogo wa soka wakioneshana ubabe.

Mapema kabisa, KMC FC waliendelea kubaki kwenye wakati mgumu baada ya kupokea kichapo cha mabao 3-2 kutoka kwa Fountain Gate FC katika mchezo uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.

Kipigo hicho kinaendelea kuwaweka KMC katika hatari kubwa ya kushuka daraja huku wakisalia mkiani mwa msimamo wa ligi. Licha ya kuonyesha ushindani katika baadhi ya dakika za mchezo huo, Fountain Gate walikuwa makini zaidi kutumia nafasi walizozipata.

Katika mchezo mwingine, Pamba Jiji FC walilazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mechi iliyokuwa na ushindani mkubwa lakini ikakosa ubora wa kumalizia nafasi langoni.

Wakati huo huo, Simba SC wametoa tamko zito baada ya kuitandika Tanzania Prisons mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa KMC Complex.

Tangu dakika za mwanzo, Simba walionyesha dhamira ya kutaka ushindi mkubwa huku wakitawala mchezo kwa kiwango kikubwa. Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa Wekundu wa Msimbazi kuwa mbele kwa mabao 3-0 yaliyofungwa na Morice Abraham, Clatous Chama na Suleiman Mwalimu.

Kipindi cha pili Simba waliendelea kushambulia kwa kasi, huku Ismail Toure akiandika bao la nne lililohitimisha karamu ya mabao kwa Simba.

Ushindi huo ungeweza kuwa mkubwa zaidi kama Simba wangekuwa makini kutumia nafasi nyingi walizozitengeneza mbele ya lango la Prisons.

Kwa ushindi huo, Simba wamefikisha alama 49 na kuendelea kujiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi, huku tofauti ya pointi dhidi ya vinara Yanga ikibaki kuwa alama tano.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →