Simba yaifumua Prisons 4-0, KMC mambo magumu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th May 2026


Simba yaifumua Prisons 4-0, KMC mambo magumu

Mikiki mikiki ya Ligi Kuu NBC imeendelea leo kwa michezo mitatu kupigwa katika viwanja tofauti huku vigogo wa soka wakioneshana ubabe.

Mapema kabisa, KMC FC waliendelea kubaki kwenye wakati mgumu baada ya kupokea kichapo cha mabao 3-2 kutoka kwa Fountain Gate FC katika mchezo uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.

Kipigo hicho kinaendelea kuwaweka KMC katika hatari kubwa ya kushuka daraja huku wakisalia mkiani mwa msimamo wa ligi. Licha ya kuonyesha ushindani katika baadhi ya dakika za mchezo huo, Fountain Gate walikuwa makini zaidi kutumia nafasi walizozipata.

Katika mchezo mwingine, Pamba Jiji FC walilazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mechi iliyokuwa na ushindani mkubwa lakini ikakosa ubora wa kumalizia nafasi langoni.

Wakati huo huo, Simba SC wametoa tamko zito baada ya kuitandika Tanzania Prisons mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa KMC Complex.

Tangu dakika za mwanzo, Simba walionyesha dhamira ya kutaka ushindi mkubwa huku wakitawala mchezo kwa kiwango kikubwa. Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa Wekundu wa Msimbazi kuwa mbele kwa mabao 3-0 yaliyofungwa na Morice Abraham, Clatous Chama na Suleiman Mwalimu.

Kipindi cha pili Simba waliendelea kushambulia kwa kasi, huku Ismail Toure akiandika bao la nne lililohitimisha karamu ya mabao kwa Simba.

Ushindi huo ungeweza kuwa mkubwa zaidi kama Simba wangekuwa makini kutumia nafasi nyingi walizozitengeneza mbele ya lango la Prisons.

Kwa ushindi huo, Simba wamefikisha alama 49 na kuendelea kujiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi, huku tofauti ya pointi dhidi ya vinara YangaΒ ikibaki kuwa alama tano.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’