International,Normal News,Arsenal, West Ham, Local

VAR yaokoa alama tatu za Arsenal dhidi ya West Ham

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 May 2026
VAR yaokoa alama tatu za Arsenal dhidi ya West Ham

Arsenal FC wameendelea kuweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya West Ham United katika mchezo wenye drama kubwa ya VAR uliopigwa London Stadium.

Mchezo huo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili huku Arsenal wakihitaji ushindi ili kuendelea kuishinikiza mbio za ubingwa. Bao pekee la ushindi lilifungwa na Leandro Trossard dakika ya 83 baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Martin Odegaard.

Dakika za mwisho za mchezo ziligeuka kuwa gumzo baada ya West Ham kuamini kuwa wamepata bao la kusawazisha kupitia Callum Wilson katika muda wa nyongeza. Hata hivyo, baada ya ukaguzi mrefu wa VAR, mwamuzi Chris Kavanagh aliamua kulikataa bao hilo kutokana na faulo dhidi ya kipa wa Arsenal David Raya kwenye harakati za kuwania mpira wa kona.

Uamuzi huo umeibua mjadala mkubwa England, huku baadhi ya wachambuzi wakidai ilikuwa moja ya maamuzi makubwa zaidi ya VAR katika mbio za ubingwa wa Premier League msimu huu.

Kwa ushindi huo, Arsenal wameendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi na kuongeza matumaini ya kutwaa ubingwa wao wa kwanza wa Premier League tangu mwaka 2004.

Arsenal wamefikisha alama 79 wakisalia na mechi mbili huku Man City wakiwa na alama 74 na mechi tatu mkononi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’