Hesabu kali zinapigwa na makocha pamoja na wachezaji katika mechi za Ligi Kuu Bara zinazotarajiwa kuchezwa mikoa tofauti leo Jumanne, ambapo Singida Black Stars itakuwa nyumbani dhidi ya Namungo kwenye Uwanja wa Airtel, huku TRA United ikiikaribisha JKT Tanzania kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, huku kila timu ikiwania nafasi ya kupanda juu kwenye msimamo.





