Okello anukia ligi kuu ya Uturuki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th May 2026


Okello anukia ligi kuu ya Uturuki

Maafisa wa klabu ya Uturuki, Fenerbahce S.K., wameripotiwa kuwepo nchini Tanzania kwa muda wa siku nne wakimfuatilia kiungo mshambuliaji wa Young Africans S.C, Allan Okello.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwanahabari wa Uganda, Ronnie Santos Mwine, wageni hao kutoka Uturuki wamevutiwa na kiwango cha mchezaji huyo wa kimataifa wa Uganda ambaye ameonyesha makali tangu ajiunge na Yanga katika dirisha dogo la usajili.

Okello ameanza maisha yake mapya kwa kishindo, akiwa tayari amechangia mabao matano na kutoa pasi za mabao saba kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, jambo lililomfanya kuwa miongoni mwa wachezaji wanaofuatiliwa kwa karibu.

Inaelezwa kuwa maafisa wa Fenerbahce wanatarajiwa kuwepo uwanjani kesho wakati Yanga itakapovaana na Dodoma Jiji FC katika mchezo wa ligi utakaopigwa kwenye Uwanja wa Airtel Mtipa mkoani Singida.

Iwapo klabu hiyo ya Uturuki itaamua kumsajili Okello, itawalazimu kufungua mazungumzo rasmi na Yanga, ingawa hadi sasa hakuna mazungunzo yaliyoanza kati ya pande hizo mbili.

Okello alijiunga na Yanga akitokea Vipers SC ya Uganda, akisaini mkataba wa miaka miwili na nusu, na sasa anaendelea kuonyesha mchango mkubwa katika kikosi hicho cha Jangwani.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’