Local,Normal News,Yanga, Dodoma Jiji

Moalin apania alama tatu dhidi ya Dodoma Jiji

Joel JJ By Joel JJ
12 May 2026
Moalin apania alama tatu dhidi ya Dodoma Jiji

Kocha Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moalin, amesema maandalizi ya kikosi chake kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Dodoma Jiji FC yamekamilika kikamilifu, huku akisisitiza dhamira ya kupata pointi tatu muhimu.

Yanga inatarajiwa kushuka dimbani Jumatano katika Uwanja wa Airtel uliopo mkoani Singida, katika mchezo ambao una umuhimu mkubwa kwa vinara hao wa ligi wanaotafuta kujiimarisha zaidi kileleni mwa msimamo.

Moalin amesema kikosi chake kipo katika hali nzuri, isipokuwa beki Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’ ambaye bado yuko chini ya uangalizi wa madaktari baada ya kurejea mazoezini akitokea kwenye majeraha.

Kocha huyo amekiri kuwa anatarajia mchezo mgumu dhidi ya Dodoma Jiji, lakini akasisitiza kuwa ana imani kubwa na ubora wa kikosi chake pamoja na maandalizi waliyofanya.

Ameongeza kuwa mazingira ya Uwanja wa Airtel yanaweza kuwapa faida kutokana na kufanana na Uwanja wa KMC Complex ambao Yanga wamekuwa wakitumia kama moja ya viwanja vyao vya nyumbani msimu huu.

Moalin amesema kila mchezo uliosalia msimu huu ni wa muhimu na hawana budi kucheza kwa tahadhari kubwa huku lengo likiwa moja tu—ushindi.

“Maandalizi yamekuwa mazuri. Mzunguko kati ya mechi ni mfupi sana, hivyo tulilazimika kuhakikisha wachezaji wanapata muda wa kupumzika na kuwa tayari kwa mchezo wa kesho. Tunatarajia mchezo mgumu lakini tumejiandaa,” alisema Moalin.

“Utakuwa mchezo wenye ushindani mkubwa dhidi ya Dodoma Jiji. Tunaamini mazingira ya uwanja yatatusaidia kwa kiasi fulani. Pamoja na ratiba ngumu, tunalenga pointi tatu.”

“Wachezaji wote wako salama isipokuwa Mohammed Hussein ambaye tunaendelea kumfuatilia. Pia Mudathir amerejea kikosini baada ya kumaliza adhabu yake ya kusimamishwa. Kila mchezo uliobaki ni muhimu sana kwetu,” aliongeza.

Yanga itaingia uwanjani ikiwa na lengo la kuendeleza ubabe wake kileleni mwa ligi, huku presha ya mbio za ubingwa ikiendelea kupamba moto.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →