Goncalves, Okello watwaa tuzo za ligi kuu April

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th May 2026


Goncalves, Okello watwaa tuzo za ligi kuu April

Kiungo mshambuliaji wa Young Africans, ALLAN OKELLO, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku PEDRO GONCALVES wa Young Africans, akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Okello alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo akiwashinda Pacome Zouzoua wa Yanga na Idd Selemani wa Azam FC, alioingia nao fainali katika mchakato wa tuzo za mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mchezaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa timu yake katika michezo mitatu aliyocheza mwezi huo, akifunga bao moja na kuhusika na mengine sita kwa dakika 320 alizocheza.

Kwa upande wa Pedro aliyeingia fainali na Steve Barker wa Simba na Etiene Ndairagije wa TRA United, aliiongoza Young Africans kushinda michezo yote mitatu iliyocheza mwezi huo na kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, ikifunga mabao 12 na haikuruhusu bao. Young Africans ilizifunga Tanzania Prisons (3-0), Mbeya City (6-0) na Pamba Jiji (0-3).

Wakati huohuo Kamati ya Tuzo, imemchagua HASSAN MWATEREMA wa Kagera Sugar kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Aprili wa Ligi ya Championship ya NBC 2025/26, huku JUMA KASEJA pia wa Kagera Sugar akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mwaterema aliyeingia fainali na Japhet Mayungu wa TMA na Salum Mlemwa wa Gunners, alionesha kiwango chenye mwendelezo, ikiwa ni pamoja na kufunga mabao mawili kwa dakika 139 za michezo miwili aliyocheza.

Kwa upande wa Kaseja aliyeingia fainali na Zuberi Katwila wa Geita Gold na Mbwana Makata wa Polisi Tanzania, aliiongoza timu yake kushinda michezo yote miwili iliyocheza mwezi huo ikiendelea kubaki nafasi ya pili.

Pia Kamati ya Tuzo imeteua MAGOLI MATATU BORA ambayo yatapigiwa kura na mashabiki ili kupata goli bora la mwezi la mashabiki. Magoli hayo ni Pacome Zouzoua (Young Africans vs Mbeya City dakika ya 43), Idd Kipagwile (Dodoma vs Fountain Gate dakika ya 68) na Grayson Gwalala (Coastal v Dodoma Jiji dakika ya 14).


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’