Local,Normal News,Simba, Yanga

Simba kupunguza gap la pointi dhidi ya Yanga Kigoma?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 May 2026
Simba kupunguza gap la pointi dhidi ya Yanga Kigoma?

Baada ya Yanga kukubali kipigo cha mabao 3-2 dhidi ya Dodoma Jiji, wamewapa nafasi watani zao Simba kuwasogelea karibu zaidi kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu msimu huu.

Simba leo itakuwa ugenini mkoani Kigoma kuikabili Mashujaa Fc katika mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali.

Alama tatu kwa Mnyama zitamaanisha Wekundu hao wa Msimbazi watafikisha alama 52 na hivyo kuwa tofauti ya alama mbili tu dhidi ya Yanga ambao bado iko kileleni ikiwa na alama 54 baada ya mechi 23.

Simba ilitua Kigoma jioni ya Jumatano timu hiyo ikikamilisha maandalizi yake yote kuelekea mchezo huo jijini Dar es salaam.

Kocha Msaidizi wa Simba Suleiman Matola amesema wanatambua Mashujaa Fc sio timu nyepesi hasa inapocheza katika uwanja wao wa nyumbani lakini wamejipanga kuhakikisha wanaondoka na alama zote tatu.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’