International,Normal News,Manchester City, Crystal Palace, Local

Man City yaendelea kuibana Arsenal ubingwa EPL

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 May 2026
Man City yaendelea kuibana Arsenal ubingwa EPL

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England, Manchester City, wameendelea kuweka presha kubwa kwa vinara Arsenal baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace usiku wa Jumatano, Mei 13, 2026.

Katika mchezo huo uliopigwa dimba la Etihad, City walionyesha ubora mkubwa tangu kipindi cha kwanza huku Antoine Semenyo, Omar Marmoush na Savinho wakifunga mabao yaliyowapa ushindi muhimu sana kwenye mbio za ubingwa wa Premier League.

Baada ya ushindi huo, kikosi cha Pep Guardiola sasa kimefikisha alama 77 katika nafasi ya pili, nyuma ya Arsenal wenye alama 79 huku timu zote zikibakiwa na mechi mbili pekee kumaliza msimu.

Kiungo Phil Foden alikuwa nyota wa mchezo baada ya kutoa pasi mbili za mabao katika kipindi cha kwanza na kuiongoza City kucheza soka la kuvutia licha ya Guardiola kuwapa mapumziko baadhi ya nyota wake akiwemo Erling Haaland kuelekea fainali ya FA Cup mwishoni mwa wiki.

Guardiola amesema timu yake bado ipo hai kwenye mbio za ubingwa na itaendelea kupambana hadi mwisho wa msimu. Kocha huyo ana matumaini Arsenal wanaweza kupoteza pointi katika mechi zao mbili zilizobaki dhidi ya Burnley na Crystal Palace.

Kwa sasa, City wanahitaji kushinda mechi zao zote zilizobaki dhidi ya Bournemouth na Aston Villa huku wakisubiri makosa kutoka kwa Arsenal ili waweze kutwaa taji hilo kwa mara nyingine.Β 

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’