Inter watwaa taji la pili ndani ya wiki

Joel JJ By Joel JJ • 14th May 2026


Inter watwaa taji la pili ndani ya wiki

Inter Milan wameendelea kuthibitisha ubabe wao nchini Italia baada ya kutwaa taji la 10 la Coppa Italia kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Lazio katika fainali iliyochezwa usiku wa Jumatano, Mei 13, 2026 kwenye dimba la Stadio Olimpico mjini Rome.

Mabingwa hao wa Serie A waliingia uwanjani wakiwa na morali kubwa baada ya tayari kutwaa Scudetto wiki iliyopita, na walionyesha ubora wao mapema kabisa kwenye mchezo huo.

Bao la kwanza lilitokana na kujifunga kwa Adam Marusic dakika ya 14 baada ya mpira wa kona wa Federico Dimarco kuleta taharuki ndani ya eneo la Lazio. Lautaro Martinez akaongeza bao la pili dakika ya 35 akimalizia pasi ya Marcus Thuram.

Ushindi huo umeifanya Inter kukamilisha “Domestic Double” yaani kutwaa Serie A pamoja na Coppa Italia ndani ya msimu mmoja. Hii ni mara ya kwanza kwa klabu ya Italia kufanya hivyo tangu Juventus msimu wa 2017–18.

Kocha mkuu Cristian Chivu ameandika historia kubwa katika msimu wake wa kwanza kuinoa Inter. Nahodha Lautaro Martinez amesema mafanikio hayo yametokana na nidhamu, umoja na hamu kubwa ya kushinda waliyoionyesha wachezaji wote msimu mzima.

Inter walitawala karibu kila eneo la mchezo huo huku kiungo Nicolò Barella na beki Denzel Dumfries wakitoa kiwango kikubwa. Lazio walijaribu kurejea kipindi cha pili kupitia Tijjani Noslin na Boulaye Dia lakini kipa Josep Martinez aliokoa hatari kadhaa muhimu.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →