Local,Normal News,Simba, Mashujaa, Mtibwa, Prisons

Simba yaunguruma Kigoma, yapunguza gap la pointi dhidi ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 May 2026
Simba yaunguruma Kigoma, yapunguza gap la pointi dhidi ya Yanga

Klabu ya Simba SC imeendelea kuonyesha makali yake kwenye mbio za ubingwa baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa dimba la Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

Mnyama aliingia uwanjani akiwa na lengo moja tu, kuondoka na alama tatu muhimu, na haukusubiri muda mrefu kuonyesha ubora wake. Ilikuwa ni dakika ya tano pekee ambapo kiungo mahiri Clatous Chama alipoinyanyua Simba kwa bao la mapema kupitia kona ya moja kwa moja iliyomshinda mlinda lango wa Mashujaa FC.

Baada ya bao hilo, Simba iliendelea kutawala mchezo kwa kiwango kikubwa huku Mashujaa FC wakionekana kuzidiwa kasi na mbinu za wekundu hao wa Msimbazi. Mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa Simba yaliwapa wakati mgumu wenyeji hao ambao walijikuta wakilazimika kucheza zaidi eneo lao la kujilinda.

Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika, Simba ilikuwa mbele kwa bao 1-0 huku mashabiki wake wakionekana kufurahia kiwango bora kilichoonyeshwa na timu yao.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ile ile kutoka kwa Simba, na tena alikuwa ni Chama aliyetikisa nyavu kwa mara ya pili kupitia shuti kali nje kidogo ya eneo la hatari. Bao hilo lilizidi kuthibitisha ubora wa kiungo huyo ambaye sasa ameweka rekodi ya kufunga mabao manne mfululizo kwenye ligi huku akifikisha mabao nane msimu huu.

Bao la tatu na la kufunga mchezo lilifungwa dakika za lala salama na Suleiman Mwalimu baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Neo Maema, akihitimisha usiku mzuri kwa Simba.

Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha alama 52 kwenye msimamo wa ligi, ikiwa nyuma kwa tofauti ya alama mbili pekee dhidi ya watani zao Young Africans SC katika mbio kali za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kwa upande mwingine, Clatous Chama aliendelea kuwa gumzo baada ya kutwaa tena tuzo ya nyota wa mchezo, ikiwa ni mara yake ya nne mfululizo kufanya hivyo, jambo linaloonyesha kiwango chake bora ndani ya kikosi cha Simba kwa sasa.

Mapema mechi nyingine zilipigwa Mtibwa Sugar wakiibuka na ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya KMC katika mchezo ambao mabao 7 yalishuhudiwa huku Tanzania Prisons nayo ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Fountain Gate na kufufua matumaini ya kwenye mapambano ya kujinusuru kushuka daraja.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’