Local,Normal News,Yanga

Yanga yazindua rasmi mradi wa ujenzi wa uwanja Jangwani

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 May 2026
Yanga yazindua rasmi mradi wa ujenzi wa uwanja Jangwani

Young Africans SC imezindua rasmi mradi mkubwa wa ujenzi wa uwanja wake mpya utakaojengwa eneo la Jangwani, Dar es Salaam, baada ya kuingia makubaliano ya ubia wa umiliki wa uwanja kwa uwiano wa asilimia 50 kwa 50 na GSM Group.

Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, ametangaza hatua hiyo muhimu kwa mabingwa hao wa soka nchini, akieleza kuwa klabu imeingia makubaliano ya kihistoria ambayo yataweka msingi mpya wa maendeleo ya miundombinu ya michezo nchini.

Ubia wa 50-50 kati ya Yanga na GSM Group

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo iliyofanyika Makao Makuu ya Yanga, Jangwani jijini Dar es Salaam, Hersi alisema klabu itatoa ardhi kwa ajili ya mradi huo, huku GSM Group ikichangia uwekezaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa kisasa.

“Nathibitisha rasmi leo kuwa Young Africans S.C. imeingia katika makubaliano ya ubia wa umiliki wa uwanja wetu mpya kwa uwiano wa asilimia 50 kwa 50 na GSM Group.”

Aidha alieleza kushukuru mchango wa Ghalib Said Mohamed kwa uamuzi wake wa kuweka usawa katika umiliki wa mradi huo mkubwa, licha ya kuwa ndiye anayechangia sehemu kubwa ya uwekezaji wa kifedha.

“Tunamshukuru kwa dhati Ghalib Said Mohamed kwa moyo wake wa kizalendo na uamuzi wake wa kuweka usawa katika umiliki wa mradi huu mkubwa, licha ya kuwa yeye ndiye anayechangia sehemu kubwa zaidi ya uwekezaji wa kifedha.”

Kwa upande wa klabu, Yanga itatoa ardhi huku GSM Group ikiwa mwekezaji mkuu wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo wa kisasa.

“Kwa upande wa klabu, Young Africans S.C. itatoa ardhi kwa ajili ya mradi huo, huku mchango wa GSM Group ukiwa ni uwekezaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo wa kisasa,” alisema Hersi.

Uwanja kukamilika ndani ya miezi 18 hadi 20

Hersi pia alibainisha kuwa mradi wa ujenzi wa uwanja huo unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miezi 18 hadi 20, na kuwa sehemu ya historia mpya ya klabu hiyo kongwe nchini Tanzania.

“Matarajio yetu ni kwamba ujenzi wa uwanja huu utakuwa umekamilika na kuzinduliwa rasmi ndani ya kipindi cha miezi 18 hadi 20 ijayo.”

Aliongeza kuwa klabu ina imani kubwa kuwa mradi huo utakamilika kwa wakati na utakuwa alama muhimu ya maendeleo ya Yanga.

“Tuna imani na matumaini makubwa kwamba mradi huu utakamilika kwa wakati uliopangwa na kuwa sehemu muhimu ya historia ya klabu yetu.”

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’