Macho ya mashabiki wa soka leo yataelekezwa katika dimba la Wembley ambapo vigogo wa England, Chelsea FC na Manchester City, watashuka dimbani kuwania ubingwa wa Kombe la FA msimu wa 2025/26.
Mchezo huo wa fainali unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikiwa na sababu tofauti ya kusaka ushindi mbele ya maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanjani hapo.





