Manchester City na Chelsea kulisaka taji la FA, fainali leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th May 2026


Manchester City na Chelsea kulisaka taji la FA, fainali leo

Macho ya mashabiki wa soka leo yataelekezwa katika dimba la Wembley ambapo vigogo wa England, Chelsea FC na Manchester City, watashuka dimbani kuwania ubingwa wa Kombe la FA msimu wa 2025/26.

Mchezo huo wa fainali unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikiwa na sababu tofauti ya kusaka ushindi mbele ya maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanjani hapo.

Manchester City wanaonolewa na Pep Guardiola wanaingia kwenye mchezo huo wakisaka kuondoa kumbukumbu mbaya ya kupoteza fainali mbili zilizopita za mashindano hayo. City wamefanikiwa kufika fainali ya FA Cup kwa mara ya nne mfululizo, rekodi mpya katika historia ya klabu hiyo.

Licha ya kuwa miongoni mwa timu zilizoonesha kiwango bora msimu huu, Guardiola amesema ratiba ngumu ya mechi imeathiri maandalizi ya kikosi chake kuelekea pambano hilo muhimu.

Kwa upande wa Chelsea, mchezo huo unaonekana kuwa nafasi muhimu ya kuokoa msimu baada ya kushindwa kufanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali msimu huu.

Chelsea hawajatwaa taji la FA Cup tangu mwaka 2018 na pia wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa hawajapata ushindi dhidi ya Manchester City katika michezo 13 iliyopita.

Kocha wa muda wa Chelsea, Calum McFarlane, amesema kikosi chake kina morali ya kufanya vizuri licha ya wengi kuwapa nafasi ndogo ya kushinda mchezo huo.

Timu hiyo pia imepata habari njema baada ya baadhi ya nyota wake waliokuwa majeruhi kurejea kikosini kuelekea mchezo huo wa mwisho wa msimu.

Kwa mujibu wa takwimu za Chama cha Soka England (FA), hii ndiyo mara ya kwanza kwa Chelsea na Manchester City kukutana kwenye fainali ya FA Cup.

Chelsea wanatafuta ubingwa wao wa tisa wa mashindano hayo huku Manchester City wakisaka taji lao la nane.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’