Azam TV yapata haki ya kurusha mechi zote kombe la Dunia 2026

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th May 2026


Azam TV yapata haki ya kurusha mechi zote kombe la Dunia 2026

Katika hatua kubwa ya kihistoria kwa tasnia ya utangazaji nchini, kituo cha televisheni cha Azam TV kimepata haki ya kipekee ya kurusha mubashara mechi zote 104 za Fainali za Kombe la Dunia 2026 zitakazofanyika katika mataifa ya Canada, Marekani na Mexico kuanzia Juni 11 hadi Julai 19.

Hii ni mara ya kwanza kwa kituo cha televisheni cha Tanzania kuonesha moja kwa moja mechi zote za fainali za Kombe la Dunia tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo makubwa ya soka duniani mwaka 1930. Pia ni mara ya kwanza kwa Azam TV yenyewe, iliyoanzishwa mwaka 2013, kupata haki ya aina hiyo ya kipekee katika historia ya kampuni hiyo.

Azam TV itaonesha mechi hizo kupitia chaneli zake za Azam Sports 2HD na Azam Sports 4HD, kuanzia mchezo wa ufunguzi utakaowakutanisha Afrika Kusini na Mexico Juni 11, hadi kilele cha mashindano hayo kitakachofanyika Julai 19, 2026.

Mashindano ya mwaka huu yanafanana kwa kuvutia na historia ya Kombe la Dunia 2010 lililofanyika Afrika Kusini, ambapo mchezo wa ufunguzi uliwakutanisha Afrika Kusini na Mexico, tukio ambalo pia litarudiwa katika toleo la 2026.

Azam TV imesema itaweka uzito mkubwa katika ubora wa matangazo kwa kutumia lugha mbili tofauti. Kwa watazamaji wa Tanzania, mechi zote zitarushwa kwa lugha ya Kiswahili fasaha, zikiambatana na uchambuzi wa kina kutoka kwa wachambuzi na watangazaji mahiri wa soka nchini.

Kwa watazamaji wa nchi jirani kama Malawi, Kenya na Uganda, matangazo yatakuwa kwa lugha ya Kiingereza, yakitolewa na timu ya watangazaji na wachambuzi kutoka nchi mbalimbali za ukanda huo.

Aidha, Azam TV imeeleza kuwa itakuwa na studio mbili za kisasa moja kwa ajili ya matangazo ya Kiswahili na nyingine kwa Kiingereza ili kuhakikisha watazamaji wote wanapata uchambuzi wa kina na ubora wa hali ya juu katika kila mchezo.

Hatua hiyo inatajwa kuwa mapinduzi makubwa katika sekta ya burudani na michezo Afrika Mashariki, huku watazamaji wakitarajiwa kufurahia moja ya matukio makubwa zaidi ya soka duniani kupitia jukwaa la ndani lenye ubora wa kimataifa.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’