Local,Normal News,Simba, TRA

TRA United yapoteana mbele ya Simba, yachapwa 4-0 robo fainali CRDB Cup

Joel JJ By Joel JJ
17 May 2026
TRA United yapoteana mbele ya Simba, yachapwa 4-0 robo fainali CRDB Cup

Klabu ya Simba SC imeonyesha ubora mkubwa na kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la CRDB baada ya kuichapa TRA United mabao 4-0 katika mchezo wa robo fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Simba ilianza mchezo huo kwa kasi kubwa huku ikifanikiwa kupata bao la mapema dakika ya tano kupitia kiungo mshambuliaji Clatous Chama ‘Mwamba wa Lusaka’ aliyemalizia kwa ustadi krosi safi kutoka kwa Nickson Kibabage.

Bao hilo limeendelea kuthibitisha kiwango bora cha Chama ambaye sasa amefunga mabao sita katika michezo mitano mfululizo akiwa katika kiwango cha juu cha kuzitikisa nyavu.

Baada ya bao hilo, Simba iliendelea kulitawala dimba kwa kucheza soka la kushambulia huku TRA United wakionekana kushindwa kuhimili presha ya wekundu hao wa Msimbazi.

Alikuwa ni kiungo mshambuliaji Anicet Oura aliiongezea Simba bao la pili kwa shuti kali la mbali lililotokana na pasi ya Alassane Kante, na kufanya Simba kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili kocha wa Simba, Steve Barker, alifanya mabadiliko kadhaa kwa kuwatoa Clatous Chama na Oura huku akiwaingiza Suleiman Mwalimu pamoja na Inno Loemba ili kuongeza nguvu mpya kikosini.

Mabadiliko hayo yalizaa matunda baada ya Suleiman Mwalimu kuandika bao la tatu kwa kuunganisha krosi nzuri ya David Kameta ‘Duchu’ ambaye alikuwa na kiwango bora na kufanikiwa kutoa asisti mbili katika mchezo huo.

Kinda Bashiri Kibaila naye alijitokeza kuhitimisha karamu ya mabao kwa kufunga bao la nne lililoweka muhuri wa ushindi mnono kwa Simba.

Kutokana na ushindi huo, Simba sasa imefuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ambapo itakutana na Coastal Union katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Ushindi huo pia unaendelea kuonyesha dhamira ya Simba kupigania kutwaa taji la CRDB Cup msimu huu huku safu yao ya ushambuliaji ikiendelea kuwa tishio kwa wapinzani.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
7h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →