Coastal Union yapania alama tatu dhidi ya Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th May 2026


Coastal Union yapania alama tatu dhidi ya Simba

Kuna dakika 180 zitapigwa kati ya Simba dhidi ya Coastal Union maarufu wagosi wa Kaya. Kabla ya timu hizo kukutana kwenye mchezo wa nusu fainali kombe la CRDB, Alhamisi May 21 zitakutana kwenye mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Coastal Union watakuwa wenyeji wa mchezo huo wa ligi ambao utapigwa uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

Wakipambana kujiweka katika nafasi nzuri ili kuepuka kushuka daraja, Coastal Union wametamba kuchukua alama tatu.

Mapema tu wametangaza viingilio vya mchezo huo utakaopigwa saa 12 jioni.

Hata hivyo haitakuwa kazi rahisi mbele ya kikosi cha Simba kinachonolewa na kocha Steve Barker ambaye ni kama ameshajipata.

Barker hajapoteza mchezo wowote wa ligi tangu alipoanza kuinoa Simba mwishoni mwa Disemba 2025.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’