Local,Normal News,Yanga, Azam

Yanga, Azam Fc kuna dakika 180 za kibabe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 May 2026
Yanga, Azam Fc kuna dakika 180 za kibabe

Msimu huu wa mashindano mbalimbali umeendelea kuonyesha ushindani mkali kati ya vigogo wa soka la Tanzania, Yanga SC na Azam FC, ambao tayari wamekutana mara mbili katika Ligi Kuu na Kombe la Muungano.

Katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC, timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana, kila moja ikijilinda na kupima nguvu za mpinzani wake. Hata hivyo, katika Kombe la Muungano, Yanga SC ilionyesha ubabe kwa kushinda mabao 2-1 dhidi ya Azam FC, matokeo yaliyowapeleka fainali ambayo hata hivyo walipoteza kwa bao 1-0 dhidi ya watani zao Simba .

Sasa bado kuna “dakika nyingine 180 za Derby ya Dar es salaam” timu hizo zikitarajiwa kukutana tena katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la CRDB. Mshindi wa pambano hilo atafuzu kwenda fainali kukutana na atakayeshinda kati ya Simba SC na Coastal Union

Aidha, safari yao bado haijaisha kabisa, kwani pia hawajakamilisha mechi ya duru ya pili ya Ligi Kuu ya NBC, ambapo Yanga SC watakuwa wenyeji wa Azam FC.

Mechi hizi mbili zinazotarajiwa kupigwa mwezi Juni 2026, zikitarajiwa kuwa mechi za kusisimua, zenye ushindani wa hali ya juu ambazo zinaweza kuamua hatma ya mataji kwa timu zote msimu huu.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’