International,Transfer News,Real Madrid, Benfica, Local

Mourinho, Real Madrid makubaliano yamefikiwa, asubiri kutambulishwa

Joel JJ By Joel JJ
18 May 2026
Mourinho, Real Madrid makubaliano yamefikiwa, asubiri kutambulishwa

Kocha maarufu wa soka duniani, José Mourinho, ameripotiwa kufikia makubaliano ya kurejea katika klabu ya Real Madrid, kwa mujibu wa taarifa za mwandishi wa usajili, Fabrizio Romano.

Romano ameripoti kuwa Mourinho na uongozi wa Real Madrid wamekubaliana masharti yote ya mkataba mpya, huku hatua iliyosalia ikiwa ni kusaini nyaraka rasmi ndani ya mwezi huu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkataba huo unatarajiwa kuwa wa awali wa miaka miwili, na masharti kati ya pande hizo mbili yakikubaliwa, jambo linaloashiria nia ya dhati ya pande zote katika kurejesha ushirikiano wao.

Inaelezwa kuwa Mourinho anatarajiwa kusafiri kuelekea Madrid mara baada ya mchezo wa Real Madrid dhidi ya Athletic Bilbao, ili kuanza rasmi maandalizi ya kuanza kazi katika awamu mpya ya kikosi hicho.

Mourinho si mgeni katika klabu hiyo, kwani aliwahi kuinoa Real Madrid na kuacha alama kubwa katika historia ya timu hiyo, hasa katika ushindani wa ndani ya La Liga na michuano ya Ulaya.

Kurejea kwake kunatajwa kuwa sehemu ya mpango wa klabu hiyo kuimarisha benchi la ufundi na kuongeza ushindani katika mafanikio ya ndani na ya kimataifa.

Mashabiki wa Real Madrid sasa wanasubiri kwa hamu kuona kama kocha huyo atarejea na mafanikio yaliyowahi kumfanya kuwa mmoja wa makocha wenye heshima kubwa duniani.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6m ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE →