Mourinho, Real Madrid makubaliano yamefikiwa, asubiri kutambulishwa

Joel JJ By Joel JJ • 18th May 2026


Mourinho, Real Madrid makubaliano yamefikiwa, asubiri kutambulishwa

Kocha maarufu wa soka duniani, José Mourinho, ameripotiwa kufikia makubaliano ya kurejea katika klabu ya Real Madrid, kwa mujibu wa taarifa za mwandishi wa usajili, Fabrizio Romano.

Romano ameripoti kuwa Mourinho na uongozi wa Real Madrid wamekubaliana masharti yote ya mkataba mpya, huku hatua iliyosalia ikiwa ni kusaini nyaraka rasmi ndani ya mwezi huu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkataba huo unatarajiwa kuwa wa awali wa miaka miwili, na masharti kati ya pande hizo mbili yakikubaliwa, jambo linaloashiria nia ya dhati ya pande zote katika kurejesha ushirikiano wao.

Inaelezwa kuwa Mourinho anatarajiwa kusafiri kuelekea Madrid mara baada ya mchezo wa Real Madrid dhidi ya Athletic Bilbao, ili kuanza rasmi maandalizi ya kuanza kazi katika awamu mpya ya kikosi hicho.

Mourinho si mgeni katika klabu hiyo, kwani aliwahi kuinoa Real Madrid na kuacha alama kubwa katika historia ya timu hiyo, hasa katika ushindani wa ndani ya La Liga na michuano ya Ulaya.

Kurejea kwake kunatajwa kuwa sehemu ya mpango wa klabu hiyo kuimarisha benchi la ufundi na kuongeza ushindani katika mafanikio ya ndani na ya kimataifa.

Mashabiki wa Real Madrid sasa wanasubiri kwa hamu kuona kama kocha huyo atarejea na mafanikio yaliyowahi kumfanya kuwa mmoja wa makocha wenye heshima kubwa duniani.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →