International,Normal News,FIFA, World Cup 2026, Local

Kombe la Dunia 2026: Mayele ndani kikosi cha DR Congo

Joel JJ By Joel JJ
18 May 2026
Kombe la Dunia 2026: Mayele ndani kikosi cha DR Congo

Shirikisho la soka la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) limetangaza rasmi kikosi cha wachezaji 26 kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026, huku mshambuliaji nyota wa Pyramids Fc Fiston Mayele akijumuishwa kwenye orodha hiyo muhimu.

Kocha Sébastien Desabre ametegemea mchanganyiko wa wachezaji wenye uzoefu barani Ulaya pamoja na mastaa wanaofanya vizuri Afrika na Mashariki ya Kati, huku DR Congo ikirejea kwenye michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1974.

Mayele, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Pyramids FC ya Misri, amekuwa katika kiwango bora msimu huu baada ya kufunga mabao muhimu kwenye michuano ya ndani na ya Afrika. 

Mbali na Mayele, majina makubwa yaliyoitwa kwenye kikosi hicho ni pamoja na Yoane Wissa, Cedric Bakambu, Aaron Wan-Bissaka, Chancel Mbemba na Simon Banza. 

Kwa mujibu wa ratiba ya mashindano, DR Congo ipo kundi moja na Portugal, Colombia pamoja na Uzbekistan. Leopards wanatarajia kutumia ushindani huo kuonyesha ubora wao duniani baada ya kusubiri zaidi ya miaka 50 kurejea kwenye Kombe la Dunia.

Kikosi Kamili cha DR Congo Kombe la Dunia 2026

Makipa

  • Lionel Mpasi
  • Timothé Fayulu
  • Matthieu Epolo

Mabeki

  • Aaron Wan-Bissaka
  • Axel Tuanzebe
  • Chancel Mbemba
  • Dylan Batubinsika
  • Rocky Bushiri
  • Arthur Masuaku
  • Joris Kayembe
  • Steve Kapuadi
  • Gedeon Kalulu

Viungo

  • Samuel Moutoussamy
  • Edo Kayembe
  • Charles Pickel
  • Noah Sadiki
  • Ngal’ayel Mukau
  • Gael Kakuta

Washambuliaji

  • Fiston Mayele
  • Yoane Wissa
  • Cedric Bakambu
  • Simon Banza
  • Theo Bongonda
  • Meshack Elia
  • Nathanael Mbuku
  • Brian Cipenga

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →