Makocha wa timu za Simba SC na Coastal Union wameanza kutambiana kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa kesho Alhamisi Mei 21 katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na umuhimu wake kwa kila upande, huku timu zote mbili zikiwa na malengo tofauti lakini muhimu katika msimamo wa ligi.





