Local,Transfer News,Yanga, Wydad, Ittihad

Yanga yaanza mipango ya kumrejesha Aziz Ki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 May 2026
Yanga yaanza mipango ya kumrejesha Aziz Ki

Yanga imeingia katika hatua mpya ya mazungumzo ya kumrejesha aliyekuwa kiungo wake mshambuliaji, Stephan Aziz Ki, ambaye kwa sasa anaichezea Al Ittihad SC baada ya kuondoka Wydad AC, imefahamika.

Aziz Ki alisajiliwa na Wydad AC kutoka Yanga SC katika dirisha la usajili la msimu uliopita, lakini alidumu kwa kipindi kifupi cha takribani miezi sita kabla ya kuhamia Libya kujiunga na Al Ittihad SC katika usajili wa dirisha dogo la Januari 2026.

Taarifa zinaeleza kuwa Yanga SC imeanza mazungumzo ya siri ili kumshawishi kurejea Jangwani, huku vyanzo vikidai kuna maendeleo mazuri yanayoendelea nyuma ya pazia.

Kwa mujibu wa taarifa zisizo rasmi, Aziz Ki amekuwa akipitia changamoto za kiusalama nchini Libya, jambo linaloaminika kuchangia kuanza kufikiria kurejea Tanzania.

Aidha, sababu za kifamilia pia zimechangia msukumo huo. Nyota huyo kutoka Burkina Faso, mkewe Hamisa Mobeto yupo nchini Tanzania, hali inayomfanya atamani kuwa karibu na familia yake.

Aziz Ki na Hamisa Mobeto walifunga ndoa Februari 16, 2025 jijini Dar es Salaam. Tangu wakati huo, mchezaji huyo amekuwa akigawanya muda wake kati ya majukumu ya kikazi Libya na maisha ya kifamilia Tanzania, hali inayoripotiwa kumletea changamoto za kijamii na kisaikolojia kutokana na umbali.

Kabla ya kuondoka, Aziz Ki aliichezea Yanga SC kwa misimu mitatu ambapo aliweka rekodi ya kufunga zaidi ya mabao 50 katika mashindano mbalimbali. Pia alifanikiwa kutwaa tuzo za Mchezaji Bora (MVP) pamoja na kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Tanzania, akijijengea jina kama mmoja wa viungo washambuliaji bora kuwahi kucheza ligi ya Tanzania Bara.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’