Local,Normal News,Yanga

Kocha Yanga amtetea Mwamnyeto

Joel JJ By Joel JJ
21 May 2026
Kocha Yanga amtetea Mwamnyeto

Kocha Mkuu wa Young Africans SC, Abdihamid Moalin, amemtetea nahodha wa kikosi hicho Bakari Nondo Mwamnyeto, akisisitiza kuwa hana mashaka na uwezo wake licha ya tukio la kujifunga lililotokea katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji FC uliochezwa mkoani Singida.

Katika mchezo huo, Mwamnyeto alijikuta akiujaza mpira kimakosa wavuni wakati akijaribu kuokoa hatari langoni, tukio lililosababisha mashabiki wengi kumkosoa kupitia mitandao ya kijamii.

Hata hivyo, Kocha Moalin amesema tukio hilo halipaswi kupunguza imani kwa beki huyo, akieleza kuwa makosa ni sehemu ya mchezo wa soka na maisha kwa ujumla.

“Kila mtu anamjua Bakari Mwamnyeto ni mchezaji mkubwa na mwenye heshima kubwa, siyo tu ndani ya Yanga bali pia kwenye soka la Tanzania kwa ujumla,” alisema Moalin.

“Siwezi kujadili uwezo wake kwa sababu ni jambo ambalo lipo wazi kwa kila mtu anayefuatilia mpira. Makosa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu, siyo kwenye mpira pekee. Kama unaogopa kufanya makosa basi huwezi kuonyesha ubora wako wala kujiamini ukiwa uwanjani.”

“Wachezaji wakubwa duniani pia hufanya makosa, lakini kinachowatofautisha ni namna wanavyorudi na kupambana zaidi. Bakari ni kiongozi ndani na nje ya uwanja. Ana uzoefu mkubwa, anaipambania timu kila wakati na mchango wake kwa Yanga ni mkubwa sana,” aliongeza.

Kocha huyo ameendelea kusisitiza kuwa Mwamnyeto bado ni sehemu muhimu ya kikosi hicho na ataendelea kupewa sapoti na benchi la ufundi pamoja na viongozi wa klabu.

“Tuna imani kubwa naye na tunaendelea kumuunga mkono kwa sababu tunajua uwezo alionao na kile anachoweza kuifanya timu hii,” alihitimisha Moalin.

Licha ya presha kutoka kwa baadhi ya mashabiki baada ya tukio hilo, uongozi wa Yanga unaonekana kuendelea kusimama nyuma ya nahodha wao, ukiamini kuwa uzoefu wake bado ni muhimu katika msimu huu wa mashindano.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →