Makocha Yanga, Namungo Fc wafunguka

Joel JJ By Joel JJ • 24th May 2026


Makocha Yanga, Namungo Fc wafunguka

Kocha Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moalin, ametoa ujumbe mzito kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Namungo FC utakaopigwa kesho Jumatatu katika Uwanja wa KMC Complex, akisisitiza kuwa kikosi chake kipo tayari licha ya muda mfupi wa maandalizi.

Moalin amesema kuwa wachezaji wake wanaelewa umuhimu wa mchezo huo na malengo yao ni kuendelea kukusanya pointi tatu tatu bila kuangalia ubora wa wapinzani wao.

Amesema:

“Maandalizi ya mchezo wetu wa kesho dhidi ya Namungo yanaendelea vizuri, tuna muda mchache lakini tuna matumaini makubwa. Namungo ni timu ngumu lakini kipaumbele chetu ni alama tatu…”

“Tunatambua umuhimu wa kila mchezo, hatuogopi kufanya kazi katika mazingira yenye presha. Tunacheza kama tunavyocheza siku zote, sisi ni Yanga. Tunahitaji presha ili kutusukuma mbele zaidi…”

“Kila mchezaji anajua mashabiki na timu inataka nini… Pacome alipata majeraha kidogo mchezo uliopita lakini anaendelea vizuri… tunahitaji hamasa ya kutosha kutoka kwa mashabiki.”

Mgunda Ajibu: Tunalenga Ushindi Dhidi ya Yanga

Kwa upande mwingine, Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Mgunda amesema timu yake imejiandaa vizuri kucheza soka la ushindi dhidi ya mabingwa hao watetezi, akisisitiza kuwa wanahitaji alama tatu muhimu ili kupanda kwenye msimamo wa ligi.

Mgunda amesema mchezo huo hautakuwa rahisi, lakini wachezaji wake wako tayari kupambana kupata matokeo chanya.

Amesema:

“Tumejiandaa kucheza mchezo mzuri dhidi ya timu nzuri ya Yanga. Hautakuwa mchezo rahisi kwa sababu wao wanahitaji alama tatu na sisi tunahitaji alama tatu pia ili tusogee kutoka hapa tulipo…”


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →