International,Normal News,Real Madrid, Mourinho, Local

Uchaguzi wachelewesha utambulisho wa Mourinho Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
25 May 2026
Uchaguzi wachelewesha utambulisho wa Mourinho Real Madrid

Uchaguzi wa uongozi ndani ya klabu ya Real Madrid umesababisha kucheleweshwa kwa utambulisho wa kocha mpya, José Mourinho, ambaye alikuwa tayari kutangazwa rasmi kuchukua mikoba ya benchi la ufundi la miamba hiyo ya Hispania.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya habari vya Ulaya, Mourinho alitarajiwa kutangazwa rasmi leo kama kocha mpya wa Real Madrid, huku mipango yote ya sherehe za utambulisho ikiwa tayari imekamilika. Hata hivyo, mchakato huo umewekwa kiporo kutokana na hali ya kisiasa ndani ya klabu hiyo.

UCHAGUZI WABADILI MPANGO WA MADRID

Uongozi wa sasa chini ya Rais Florentino Pérez unakabiliwa na upinzani kutoka kwa mgombea mwingine, Enrique Riquelme, ambaye ameanzisha makao makuu ya kampeni yake karibu na Uwanja wa Santiago Bernabéu.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka Record, kama si mchakato wa uchaguzi, Mourinho angekuwa amethibitishwa rasmi kama kocha mpya wa Real Madrid.

Hata hivyo, kutokana na ushindani wa uchaguzi huo, tangazo la Mourinho limeahirishwa hadi baada ya matokeo rasmi yanayotarajiwa kutolewa tarehe 7 Juni.

MOURINHO KUSUBIRI MAAMUZI

Mourinho, ambaye aliondoka Madrid hapo awali akiwa na historia ya mafanikio na misuguano, aliondoka tena kwenda Lisbon jana akisubiri hatma yake mpya.

Kwa sasa, hatma yake ndani ya Santiago Bernabéu haijawa wazi, huku ikielezwa kuwa uteuzi wake unaweza kutegemea matokeo ya uchaguzi huo.

Endapo Florentino Pérez hatashinda uchaguzi huo, bado haijafahamika kama uongozi mpya utasonga mbele na mpango wa kumrejesha Mourinho au kuchagua kocha mwingine kabisa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →