Yanga wameonesha ubabe wao tena kwenye Ligi Kuu ya NBC baada ya kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Namungo FC katika mchezo uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.
Yanga ilianza kwa kasi ambapo Duke Abuya aliwafungia bao la mapema dakika ya 26 kupitia shambulizi la kushtukiza lililowaacha mabeki wa Namungo wakipoteana. Bao hilo liliwapa Wananchi matumaini ya mchezo mzuri.





