International,Transfer News,Manchester City, Chelsea, Local

Enzo Maresca ndiye mrithi wa Guardiola Man City

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 May 2026
Enzo Maresca ndiye mrithi wa Guardiola Man City

Habari za moto na zimethibitishwa! Kocha wa zamani wa Chelsea, Enzo Maresca atajiunga na klabu ya Manchester City kuchukua nafasi ya Pep Guardiola.

Kwa mujibu wa mwanahabari maarufu wa usajili wa soka, Fabrizio Romano kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, amefichua taarifa za β€œEXCLUSIVE” zikidai kuwa Maresca tayari amesaini mkataba wa miaka mitatu na Manchester City.

Romano ameandika kuwa makubaliano yote yamekamilika rasmi, na kwamba tangazo la Maresca kuwa kocha mpya wa City linatarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Kocha huyo anatajwa kuchukua nafasi ya Guardiola, ambaye ameiongoza City kupata mafanikio makubwa katika miaka 10, ikiwemo mataji ya Premier League na UEFA Champions League.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa Maresca amesaini mkataba unaoendelea hadi Juni 2029, hatua inayomaanisha kuwa klabu hiyo ya Etihad ina mpango wa muda mrefu wa kuendeleza falsafa yake ya soka la kumiliki mpira na mashambulizi ya kasi.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
32m ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
2h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
4h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
4h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
5h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
6h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
13h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
18h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
18h ago
READ MORE β†’