Local,Normal News,KMC, Ligi Kuu

KMC wafikia rekodi mbaya ya Kengold Fc Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 May 2026
KMC wafikia rekodi mbaya ya Kengold Fc Ligi Kuu

Klabu ya KMC FC imeifikia rasmi rekodi mbaya iliyokuwa inashikiliwa na Kengold FC ya kupoteza michezo 20 katika msimu mmoja wa Ligi Kuu ya NBC.

KMC wamefikisha idadi hiyo baada ya jana kuchapwa mabao 3-0 na Azam FC wakipoteza mechi yao ya 20 msimu huu, huku wakiwa bado na michezo mitano kabla ya kumalizika kwa msimu wa 2025/26.

Kengold waliweka rekodi hiyo misimu miwili iliyopita baada ya kupoteza mechi 20 katika michezo 30 kabla ya kushuka daraja.

Mpaka sasa KMC wamecheza mechi 25 ambapo wameshinda michezo miwili pekee, kutoka sare mara tatu na kupoteza michezo 20, hali inayozidi kuweka matumaini yao ya kubaki ligi kuu katika mazingira magumu.

Matokeo hayo yameifanya klabu hiyo kuwa katika hatari kubwa ya kushuka daraja kwenda Championship msimu ujao, huku wachambuzi wa soka wakieleza kuwa KMC wanahitaji muujiza kuweza kunusurika kushuka daraja.

Ratiba iliyosalia kwa KMC inaonyesha kuwa bado wana kazi ngumu mbele yao, ambapo watakutana na Coastal Union, TRA United, Namungo FC, Mashujaa FC pamoja na Simba SC.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’