Local,Transfer News,Coastal Union, TP Mazembe

Kiungo Coastal Union kuibukia TP Mazembe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 May 2026
Kiungo Coastal Union kuibukia TP Mazembe

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Coastal Union, Bakari Msimu, amekamilisha rasmi usajili wake wa kujiunga na vigog wa soka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, TP Mazembe, katika hatua kubwa ya maendeleo ya maisha yake ya soka.

Makubaliano kati ya Coastal Union na TP Mazembe yamefikiwa kwa mafanikio, huku nyota huyo kijana akisubiri kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2025/26 kabla ya kuanza rasmi safari yake mpya nchini DR Congo.

Msimu amekuwa mmoja wa vijana wanaotajwa kuwa na mustakabali mkubwa katika soka la Tanzania kutokana na uwezo wake wa kucheza maeneo mbalimbali, kasi, ubunifu na uwezo wa kutengeneza nafasi za mabao.

Hatua ya kujiunga na TP Mazembe inaonekana kuwa fursa muhimu kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, ambaye sasa atapata nafasi ya kuonyesha uwezo wake katika moja ya klabu kubwa na zenye historia kubwa zaidi barani Afrika.

Msimu ni sehemu ya wachezaji walioitwa kikosi cha Taif Stars kwa ajili ya mechi za kirafiki dhidi ya Rwanda na Uganda.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’