Aucho atajwa Yanga mkataba wake na Singida BS ukielekea ukingoni

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st June 2026


Aucho atajwa Yanga mkataba wake na Singida BS ukielekea ukingoni

Kiungo mkabaji wa Uganda, Khalid Aucho, ameanza kuhusishwa tena na uwezekano wa kurejea katika klabu ya Young Africans SC baada ya taarifa kueleza kuwa mkataba wake na Singida Black Stars unafikia tamati mwishoni mwa msimu huu.

Aucho ambaye alisaini mkataba wa mwaka mmoja na Singida Black Stars, anatarajiwa kuwa mchezaji huru mara tu msimu utakapomalizika. Hali hiyo inafungua milango ya vilabu mbalimbali kumwania, ikiwemo Yanga ambao waliwahi kufaidika na huduma zake kwa misimu iliyopita.

Tangu kuondoka kwake Yanga, mashabiki na wachambuzi wamekuwa wakieleza kuwa nafasi yake kwenye kiungo cha ukabaji haijapata mbadala wa kudumu. Uimara wake, uzoefu na uwezo wa kuongoza safu ya kiungo vilikuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya timu hiyo.

Baada ya kuondoka kwake, Yanga ilijaribu kuongeza nguvu kwa kumsajili Moussa Balla Conte, lakini mchezaji huyo hakupata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza. Hali hiyo ilisababisha aondoke kwa mkopo.

Baadaye, klabu hiyo ikamchukua kwa mkopo Mohamed Damaro β€œNgosha” kutoka Singida Black Stars ili kuongeza nguvu eneo la kiungo cha ukabaji.

Kwa sasa, jukumu la kiungo mkabaji ndani ya Yanga linabebwa zaidi na Duke Abuya, huku Damaro pia akipata nafasi kwa vipindi. Hata hivyo, changamoto ya kadi na majeraha imekuwa ikipunguza uthabiti wa kikosi hicho eneo hilo.

Kuna uwezekano mkubwa kwamba Yanga watarejea sokoni kusaka kiungo mkabaji wa kiwango cha juu kuelekea msimu ujao. Jina la Aucho limeanza kuibuka tena kutokana na uzoefu wake na historia yake ndani ya klabu hiyo.

Aucho aliondoka Yanga baada ya mazungumzo ya mkataba kushindikana, ambapo alitaka mkataba wa miaka miwili, huku klabu ikitoa ofa ya mwaka mmoja pekee. Tofauti hiyo ilipelekea pande hizo mbili kuachana kwa makubaliano.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’