Local,Transfer News,Simba, TRA United

Simba, Chamou mwisho umefika

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Jun 2026
Simba, Chamou mwisho umefika

Klabu ya Simba SC haina mpango wa kuendelea na beki raia wa Ivory Coast Carabou Chamou, akiwa sio sehemu ya mipango ya timu hiyo kwa msimu ujao.

Inaelezwa kuwa viongozi wa Simba tayari wamemuarifu mchezaji huyo kuhusu msimamo wa klabu, hatua inayompa nafasi ya kuanza kutafuta changamoto mpya kabla ya kufunguliwa kwa dirisha kubwa la usajili mwezi ujao.

Chamoua kwa sasa anaitumikia TRA United FC kwa mkopo, ambapo ameendelea kupata muda wa kucheza baada ya kushindwa kupata nafasi ya kudumu ndani ya kikosi cha Wekundu wa Msimbazi msimu huu.

Mkataba wa beki huyo na Simba unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi huu. Wakati huo huo, TRA United inatajwa kuridhishwa na mchango wake na inaonyesha nia ya kuendelea kuwa naye kwa muda mrefu zaidi.

Chamoua alikuwa miongoni mwa wachezaji waliosajiliwa katika msimu wa 2024/25 wakati Simba ilipoanza mchakato wa kujenga kikosi kipya chini ya kocha Fadlu Davids. Hata hivyo, ushindani mkubwa wa nafasi ndani ya kikosi ulimfanya ashindwe kupata nafasi ya mara kwa mara.

Pamoja na Chamoua, kiungo Mzamiru Yassin pia anakabiliwa na hatma inayofanana. Mchezaji huyo naye anatarajiwa kumaliza mkataba wake mwishoni mwa mwezi huu, huku taarifa zikieleza kuwa hana nafasi katika mipango ya Simba ya msimu ujao.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’