Eriksen kufanyiwa uchunguzi zaidi baada ya tukio la kuanguka tena uwanjani

Joel JJ By Joel JJ • 8th June 2026


Eriksen kufanyiwa uchunguzi zaidi baada ya tukio la kuanguka tena uwanjani

Christian Eriksen amewekwa chini ya uangalizi wa karibu wa kitabibu baada ya tukio la ghafla lililotokea uwanjani ambapo alionekana kuanguka na kupoteza fahamu kwa muda mfupi kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Denmark dhidi ya Ukraine uliopigwa Jumapili usiku huko Denmark

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na timu ya matibabu, Eriksen alipata huduma ya haraka uwanjani na hali yake ilianza kuimarika baada ya muda mfupi, ambapo fahamu zake zilirejea.

Taarifa zinaeleza kuwa Eriksen anaendelea vizuri na hali yake kwa ujumla iko chini ya uangalizi wa wataalamu. Vifaa vya kudhibiti mapigo ya moyo vilivyowekwa mwilini mwake vimeonyesha kufanya kazi kama ilivyokusudiwa, na hakuna dalili za tatizo kubwa la haraka lililogunduliwa wakati wa tukio hilo.

Hata hivyo, madaktari wamesisitiza kuwa atafanyiwa vipimo zaidi hospitalini ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo la kupoteza fahamu ghafla.

“Sasa atafanyiwa uchunguzi zaidi hospitalini ili kubaini haswa kilichosababisha kutokea tukio hilo. Tunaendelea kuwasiliana naye pamoja na madaktari wake wa karibu hospitalini,” alisema daktari wa Denmark

Pia imeelezwa kuwa Eriksen mwenyewe amekuwa na hali nzuri ya mawasiliano baada ya tukio hilo na alituma salamu kwa wachezaji wenzake akiwahakikishia kuwa yuko sawa.

“Ila Christian anaendelea vizuri, na aliniomba nitume salamu zake kwa wachezaji wote na kuwaambia kwamba yuko sawa.”


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.