Local,Transfer News,Tetesi, Simba

Camara kutua Ufaransa baada ya kuondoka Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Jun 2026
Camara kutua Ufaransa baada ya kuondoka Simba

Mlinda mlango wa Simba, Moussa Camara (27), anatarajiwa kujiunga na klabu ya FC Annecy inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini Ufaransa (Ligue 2) mara baada ya kumalizika kwa msimu huu.

Camara, raia wa Guinea, atatua katika kikosi hicho akiwa mchezaji huru kufuatia kumalizika kwa mkataba wake na Simba SC.

Taarifa zinaeleza kuwa Simba ilikuwa tayari kumuongezea mkataba golikipa huyo ili aendelee kuitumikia klabu hiyo, lakini pande zote mbili hazikufikia mwafaka wa makubaliano mapya.

Camara anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na FC Annecy mara baada ya kukamilisha taratibu za mwisho za uhamisho wake.

Safari ya Camara ndani ya Simba imekuwa ya mafanikio na changamoto kwa nyakati tofauti. Aliitumikia klabu hiyo kwa msimu mmoja kamili akiwa chaguo muhimu langoni, lakini msimu wake wa pili ulikumbwa na majeraha makubwa yaliyomuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Kutokana na majeraha hayo, Simba ilimwondoa kwenye kikosi chake wakati wa dirisha dogo la usajili na baadaye kumsajili Djibrilla Kassali kuziba pengo lake. Camara alifanyiwa upasuaji wa goti nchini Morocco mwanzoni mwa msimu huu katika jitihada za kurejea uwanjani.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’