Klabu ya Yanga inatajwa kuwa imekamilisha usajili wa mshambuliaji Yves Koutiama (27), raia wa Burkina Faso, ikiwa ni sehemu ya maboresho ya kikosi kuelekea msimu ujao wa mashindano.
Koutiama anajiunga na mabingwa hao wa Tanzania Bara baada ya kuwa na kiwango bora akiwa na Polisi FC ya Kenya, aliyoitumikia tangu dirisha dogo la usajili la msimu uliomalizika.





