Mechi ya Zanzibar dhidi ya Uganda yafutwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th June 2026


Mechi ya Zanzibar dhidi ya Uganda yafutwa

Mamlaka za soka visiwani Zanzibar imefuta mchezo wa kimataifa wa kirafiki kati ya timu ya Taifa ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes' dhidi ya Uganda uliokuwa upigwe Alhamisi uwanja wa New Amaan Complex.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema leo, mchezo huo umefutwa kutokana na sababu za kiafya.

Ikumbukwe kwa sasa Uganda imekumbwa na janga la ugonjwa wa Ebola.

Tanzania na Uganda ilikuwa zicheze mchezo wa kirafiki ndhini Morocco pia lakini mchezo huo ulifutwa pamoja na mechi nyingine kutokana na changamoto hiyohiyo.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.