International,Normal News,Raja CA, Simba, Local

Fadlu na Raja makubaliano ya pande mbili ni suala la muda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 Jun 2026
Fadlu na Raja makubaliano ya pande mbili ni suala la muda

Kocha mkuu wa klabu ya Raja Club Athletic, Fadlu Davids, yuko mbioni kuondoka katika klabu hiyo baada ya pande zote mbili kuanza mazungumzo ya kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pamoja.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, kikao kilichofanyika jana kati ya uongozi wa Raja CA na kocha huyo wa Afrika Kusini hakikufikia muafaka wa mwisho kuhusu masharti ya kuachana. Kikwazo kikubwa kimeendelea kuwa suala la fidia ya kuvunjwa kwa mkataba.

Inaelezwa kuwa Raja CA wanatarajiwa kulipa kiasi cha dola za Kimarekani 215,000 ili kusitisha mkataba wa Davids, huku mazungumzo yakiendelea ili kufikia makubaliano ya mwisho.

Pande zote mbili zinatarajiwa kukutana tena katika juhudi za kumaliza mchakato huo na kufikia mwafaka rasmi.

Ingawa hadi sasa hakuna hati yoyote iliyosainiwa rasmi, dalili zote zinaonyesha kuwa kuondoka kwa Davids katika klabu hiyo ni suala la muda tu.

Davids alichukua mikoba ya kuinoa Raja CA baada ya kuondoka Tanzania, ambako aliwahi kufanya kazi katika benchi la ufundi la Simba SC.Β 

Raja CA imefikia uamuzi wa kumfuta kazi baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo matokeo yaliyopelekea timu hiyo kushuka hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi tofauti ya alama nne dhidi ya vinara wa ligi RS Berkane.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
35m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’