Kiungo mshambuliaji wa Yanga Allan Okello amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi Mei 2026.
Okello ametwaa tuzo hiyo akiwashinda Clatous Chama wa Simba na Feisal Salum wa Azam Fc.
Katika mwezi huo Okello alifunga mabao 9 na kutoa pasi moja ya bao.

Aidha kocha wa Simba Steve Barker yeye ametangazwa kuwa kocha bora wa mwezi Mei 2026.
Katika mwezi huo Barker aliiongoza Simba kwenye mechi sita akishinda tano na kutoka sare mchezo mmoja na kuisaidia timu yake kubaki kwenye nafasi ya pili.
Barker amewabwaga Florent Ibenge wa Azam Fc na Fredy Minziro wa Fountain Gate alioingia nao fainali
Meneja wa uwanja wa Airtel, Singida Omary Malule amechaguliwa kuwa Meneja bora wa uwanja kwa Mei.



