Local,Normal News,Simba, Pamba

Kocha Simba aweka wazi mipango ya kuikabili Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Jun 2026
Kocha Simba aweka wazi mipango ya kuikabili Pamba Jiji

Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo muhimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Pamba Jiji utakaochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Akizungumza kuelekea pambano hilo, Barker amesema maandalizi ya timu yamekamilika na wachezaji wako katika hali nzuri ya kupambana kutafuta ushindi ambao ni muhimu katika mbio za ubingwa wa ligi msimu huu.

Mchezo huo utakuwa wa kwanza kati ya mechi tano zilizosalia kwa Simba, huku Wekundu wa Msimbazi wakihitaji kushinda michezo yote ili kuendelea kuweka presha kwa watani wao wa jadi Yanga kwenye kinyang'anyiro cha ubingwa.

"Sisi tuko tayari, tumepata muda mzuri wa kujipanga vyema kwa mechi hii na mechi zote zilizosalia hadi mwisho wa msimu," alisema Barker.

Kocha huyo raia wa Afrika Kusini alisisitiza kuwa lengo kuu la Simba ni kupata alama tatu licha ya kutambua kuwa watakutana na upinzani mkubwa kutoka kwa Pamba Jiji.

"Malengo yetu ni kupata alama tatu kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Pamba Jiji. Tunajua hautakuwa mchezo mwepesi," aliongeza.

"Tunajua tutakutana na upinzani mkali kutoka kwa wapinzani wetu, lakini tuko tayari kupambana na kuhakikisha tunapata ushindi kwenye mchezo huo."

Mashabiki wa Simba watakuwa na matumaini makubwa kuona timu yao ikiendeleza kasi ya ushindi na kuendelea kufukuzia ndoto ya kutwaa ubingwa hadi dakika za mwisho za msimu.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’